Swahili
Surah Al-Mulk ( Dominion ) - Aya count 30
تَبَارَكَ الَّذِي بِيَدِهِ الْمُلْكُ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ
( 1 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 1 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 1](style/islamic/icons/mp3.png)
AMETUKUKA ambaye mkononi mwake umo Ufalme wote; na Yeye ni Mwenye uweza juu ya kila kitu.
الَّذِي خَلَقَ الْمَوْتَ وَالْحَيَاةَ لِيَبْلُوَكُمْ أَيُّكُمْ أَحْسَنُ عَمَلًا ۚ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْغَفُورُ
( 2 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 2 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 2](style/islamic/icons/mp3.png)
Ambaye ameumba mauti na uhai ili kukujaribuni ni nani miongoni mwenu mwenye vitendo vizuri zaidi. Na Yeye ni Mwenye nguvu na Mwenye msamaha.
الَّذِي خَلَقَ سَبْعَ سَمَاوَاتٍ طِبَاقًا ۖ مَّا تَرَىٰ فِي خَلْقِ الرَّحْمَٰنِ مِن تَفَاوُتٍ ۖ فَارْجِعِ الْبَصَرَ هَلْ تَرَىٰ مِن فُطُورٍ
( 3 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 3 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 3](style/islamic/icons/mp3.png)
Aliye umba mbingu saba kwa matabaka. Huoni tafauti yoyote katika uumbaji wa Mwingi wa Rehema. Hebu rudisha nadhari! Unaona kosa lolote?
ثُمَّ ارْجِعِ الْبَصَرَ كَرَّتَيْنِ يَنقَلِبْ إِلَيْكَ الْبَصَرُ خَاسِئًا وَهُوَ حَسِيرٌ
( 4 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 4 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 4](style/islamic/icons/mp3.png)
Tena rudisha nadhari mara mbili, nadhari yako itakurejea mwenyewe hali ya kuwa imehizika nayo imechoka.
وَلَقَدْ زَيَّنَّا السَّمَاءَ الدُّنْيَا بِمَصَابِيحَ وَجَعَلْنَاهَا رُجُومًا لِّلشَّيَاطِينِ ۖ وَأَعْتَدْنَا لَهُمْ عَذَابَ السَّعِيرِ
( 5 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 5 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 5](style/islamic/icons/mp3.png)
Na kwa hakika tumeipamba mbingu ya karibu kwa mataa, na tumeyafanya ili kuwapigia mashetani, na tumewaandalia adhabu ya Moto uwakao kwa nguvu.
وَلِلَّذِينَ كَفَرُوا بِرَبِّهِمْ عَذَابُ جَهَنَّمَ ۖ وَبِئْسَ الْمَصِيرُ
( 6 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 6 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 6](style/islamic/icons/mp3.png)
Na kwa walio mkufuru Mola wao Mlezi ipo adhabu ya Jahannamu. Na ni marejeo maovu yalioje hayo!
إِذَا أُلْقُوا فِيهَا سَمِعُوا لَهَا شَهِيقًا وَهِيَ تَفُورُ
( 7 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 7 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 7](style/islamic/icons/mp3.png)
Watakapo tupwa humo watausikia mngurumo wake na huku inafoka.
تَكَادُ تَمَيَّزُ مِنَ الْغَيْظِ ۖ كُلَّمَا أُلْقِيَ فِيهَا فَوْجٌ سَأَلَهُمْ خَزَنَتُهَا أَلَمْ يَأْتِكُمْ نَذِيرٌ
( 8 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 8 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 8](style/islamic/icons/mp3.png)
Inakaribia kupasuka kwa hasira. Kila mara likitupwa kundi humo walinzi wake huwauliza: Kwani hakukujieni mwonyaji?
قَالُوا بَلَىٰ قَدْ جَاءَنَا نَذِيرٌ فَكَذَّبْنَا وَقُلْنَا مَا نَزَّلَ اللَّهُ مِن شَيْءٍ إِنْ أَنتُمْ إِلَّا فِي ضَلَالٍ كَبِيرٍ
( 9 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 9 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 9](style/islamic/icons/mp3.png)
Watasema: Kwani! Ametujia mwonyaji, lakini tulimkadhibisha, na tukasema: Mwenyezi Mungu hakuteremsha chochote. Nyinyi hamumo ila katika upotovu mkubwa!
وَقَالُوا لَوْ كُنَّا نَسْمَعُ أَوْ نَعْقِلُ مَا كُنَّا فِي أَصْحَابِ السَّعِيرِ
( 10 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 10 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 10](style/islamic/icons/mp3.png)
Na watasema: Lau kuwa tungeli sikia, au tungeli kuwa na akili, tusingeli kuwa katika watu wa Motoni!
فَاعْتَرَفُوا بِذَنبِهِمْ فَسُحْقًا لِّأَصْحَابِ السَّعِيرِ
( 11 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 11 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 11](style/islamic/icons/mp3.png)
Wakakiri dhambi zao. Basi kuangamia ni kwa watu wa Motoni!
إِنَّ الَّذِينَ يَخْشَوْنَ رَبَّهُم بِالْغَيْبِ لَهُم مَّغْفِرَةٌ وَأَجْرٌ كَبِيرٌ
( 12 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 12 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 12](style/islamic/icons/mp3.png)
Hakika wanao mwogopa Mola wao Mlezi kwa ghaibu, watapata maghfira na ujira mkubwa.
وَأَسِرُّوا قَوْلَكُمْ أَوِ اجْهَرُوا بِهِ ۖ إِنَّهُ عَلِيمٌ بِذَاتِ الصُّدُورِ
( 13 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 13 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 13](style/islamic/icons/mp3.png)
Na ficheni kauli zenu, au zitangazeni; hakika Yeye ni Mjuzi wa yaliyomo vifuani.
أَلَا يَعْلَمُ مَنْ خَلَقَ وَهُوَ اللَّطِيفُ الْخَبِيرُ
( 14 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 14 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 14](style/islamic/icons/mp3.png)
Asijue aliye umba, naye ndiye Mjua siri, Mwenye khabari?
هُوَ الَّذِي جَعَلَ لَكُمُ الْأَرْضَ ذَلُولًا فَامْشُوا فِي مَنَاكِبِهَا وَكُلُوا مِن رِّزْقِهِ ۖ وَإِلَيْهِ النُّشُورُ
( 15 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 15 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 15](style/islamic/icons/mp3.png)
Yeye ndiye aliye idhalilisha ardhi kwa faida yenu, basi tembeeni katika pande zake, na kuleni katika riziki zake. Na kwake Yeye ndio kufufuliwa.
أَأَمِنتُم مَّن فِي السَّمَاءِ أَن يَخْسِفَ بِكُمُ الْأَرْضَ فَإِذَا هِيَ تَمُورُ
( 16 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 16 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 16](style/islamic/icons/mp3.png)
Mnadhani mko salama kwa alioko juu kuwa hatakudidimizeni kwenye ardhi, na tahamaki hiyo inatikisika!
أَمْ أَمِنتُم مَّن فِي السَّمَاءِ أَن يُرْسِلَ عَلَيْكُمْ حَاصِبًا ۖ فَسَتَعْلَمُونَ كَيْفَ نَذِيرِ
( 17 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 17 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 17](style/islamic/icons/mp3.png)
Au mnadhani mko salama kwa alioko juu ya kuwa Yeye hakupelekeeni kimbunga chenye changarawe? Mtajua vipi maonyo yangu?
وَلَقَدْ كَذَّبَ الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ فَكَيْفَ كَانَ نَكِيرِ
( 18 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 18 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 18](style/islamic/icons/mp3.png)
Na bila ya shaka walikwisha kanusha walio kuwa kabla yao; basi kulikuwaje kukasirika kwangu?
أَوَلَمْ يَرَوْا إِلَى الطَّيْرِ فَوْقَهُمْ صَافَّاتٍ وَيَقْبِضْنَ ۚ مَا يُمْسِكُهُنَّ إِلَّا الرَّحْمَٰنُ ۚ إِنَّهُ بِكُلِّ شَيْءٍ بَصِيرٌ
( 19 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 19 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 19](style/islamic/icons/mp3.png)
Kwani hawawaoni ndege walioko juu yao namna wanavyo zikunjua mbawa zao, na kuzikunja? Hawawashikilii ila Mwingi wa rehema. Hakika Yeye ni Mwenye kuona kila kitu.
أَمَّنْ هَٰذَا الَّذِي هُوَ جُندٌ لَّكُمْ يَنصُرُكُم مِّن دُونِ الرَّحْمَٰنِ ۚ إِنِ الْكَافِرُونَ إِلَّا فِي غُرُورٍ
( 20 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 20 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 20](style/islamic/icons/mp3.png)
Au ni lipi hilo jeshi lenu la kukunusuruni badala ya Mwingi wa Rehema? Hakika makafiri hawamo ila katika udanganyifu.
أَمَّنْ هَٰذَا الَّذِي يَرْزُقُكُمْ إِنْ أَمْسَكَ رِزْقَهُ ۚ بَل لَّجُّوا فِي عُتُوٍّ وَنُفُورٍ
( 21 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 21 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 21](style/islamic/icons/mp3.png)
Au ni nani huyo ambaye atakupeni riziki kama Yeye akizuia riziki yake? Bali wao wanakakamia tu katika jeuri na chuki.
أَفَمَن يَمْشِي مُكِبًّا عَلَىٰ وَجْهِهِ أَهْدَىٰ أَمَّن يَمْشِي سَوِيًّا عَلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ
( 22 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 22 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 22](style/islamic/icons/mp3.png)
Je! Anaye kwenda akisinukia juu ya uso wake ni mwongofu zaidi, au yule anaye kwenda sawasawa katika Njia Iliyo Nyooka?
قُلْ هُوَ الَّذِي أَنشَأَكُمْ وَجَعَلَ لَكُمُ السَّمْعَ وَالْأَبْصَارَ وَالْأَفْئِدَةَ ۖ قَلِيلًا مَّا تَشْكُرُونَ
( 23 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 23 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 23](style/islamic/icons/mp3.png)
Sema: Yeye ndiye aliye kuumbeni tangu mwanzo, na akakupeni masikio na macho, na nyoyo. Ni kidogo kabisa shukrani zenu.
قُلْ هُوَ الَّذِي ذَرَأَكُمْ فِي الْأَرْضِ وَإِلَيْهِ تُحْشَرُونَ
( 24 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 24 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 24](style/islamic/icons/mp3.png)
Sema: Yeye ndiye aliye kutawanyeni katika ardhi, na kwake mtakusanywa.
وَيَقُولُونَ مَتَىٰ هَٰذَا الْوَعْدُ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ
( 25 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 25 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 25](style/islamic/icons/mp3.png)
Na wanasema: Lini ahadi hii, ikiwa mnasema kweli?
قُلْ إِنَّمَا الْعِلْمُ عِندَ اللَّهِ وَإِنَّمَا أَنَا نَذِيرٌ مُّبِينٌ
( 26 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 26 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 26](style/islamic/icons/mp3.png)
Sema: Hakika ujuzi wake uko kwa Mwenyezi Mungu; na hakika mimi ni mwonyaji tu mwenye kubainisha.
فَلَمَّا رَأَوْهُ زُلْفَةً سِيئَتْ وُجُوهُ الَّذِينَ كَفَرُوا وَقِيلَ هَٰذَا الَّذِي كُنتُم بِهِ تَدَّعُونَ
( 27 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 27 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 27](style/islamic/icons/mp3.png)
Lakini watakapo iona karibu, nyuso za walio kufuru zitahuzunishwa, na itasemwa: Hayo ndiyo mliyo kuwa mkiyaomba.
قُلْ أَرَأَيْتُمْ إِنْ أَهْلَكَنِيَ اللَّهُ وَمَن مَّعِيَ أَوْ رَحِمَنَا فَمَن يُجِيرُ الْكَافِرِينَ مِنْ عَذَابٍ أَلِيمٍ
( 28 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 28 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 28](style/islamic/icons/mp3.png)
Sema: Mwaonaje, ikiwa Mwenyezi Mungu atanihiliki mimi na walio pamoja nami, au akiturehemu, ni nani atakaye walinda makafiri na adhabu chungu?
قُلْ هُوَ الرَّحْمَٰنُ آمَنَّا بِهِ وَعَلَيْهِ تَوَكَّلْنَا ۖ فَسَتَعْلَمُونَ مَنْ هُوَ فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ
( 29 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 29 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 29](style/islamic/icons/mp3.png)
Sema: Yeye ndiye Mwingi wa Rehema; tunamuamini Yeye, na juu yake tunategemea. Mtakuja jua ni nani aliye katika upotovu ulio dhaahiri.
قُلْ أَرَأَيْتُمْ إِنْ أَصْبَحَ مَاؤُكُمْ غَوْرًا فَمَن يَأْتِيكُم بِمَاءٍ مَّعِينٍ
( 30 ) ![Swahili - Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 30 Al-Mulk ( Dominion ) - Aya 30](style/islamic/icons/mp3.png)
Sema: Mwaonaje, yakiwa maji yenu yamedidimia chini, nani atakueleteeni maji yanayo miminika?