Swahili
Surah Nooh - Aya count 28
إِنَّا أَرْسَلْنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوْمِهِ أَنْ أَنذِرْ قَوْمَكَ مِن قَبْلِ أَن يَأْتِيَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ
( 1 ) ![Swahili - Nooh - Aya 1 Nooh - Aya 1](style/islamic/icons/mp3.png)
Hakika Sisi tulimtuma Nuh'u kwa watu wake: Uwaonye kaumu yako kabla ya kuwafikia adhabu chungu.
قَالَ يَا قَوْمِ إِنِّي لَكُمْ نَذِيرٌ مُّبِينٌ
( 2 ) ![Swahili - Nooh - Aya 2 Nooh - Aya 2](style/islamic/icons/mp3.png)
Akasema: Enyi watu wangu! Kwa hakika mimi ni mwonyaji wa dhaahiri kwenu,
أَنِ اعْبُدُوا اللَّهَ وَاتَّقُوهُ وَأَطِيعُونِ
( 3 ) ![Swahili - Nooh - Aya 3 Nooh - Aya 3](style/islamic/icons/mp3.png)
Ya kwamba mumuabudu Mwenyezi Mungu, na mumche Yeye, na mumt'ii.
يَغْفِرْ لَكُم مِّن ذُنُوبِكُمْ وَيُؤَخِّرْكُمْ إِلَىٰ أَجَلٍ مُّسَمًّى ۚ إِنَّ أَجَلَ اللَّهِ إِذَا جَاءَ لَا يُؤَخَّرُ ۖ لَوْ كُنتُمْ تَعْلَمُونَ
( 4 ) ![Swahili - Nooh - Aya 4 Nooh - Aya 4](style/islamic/icons/mp3.png)
Atakughufirieni madhambi yenu, na atakuakhirisheni mpaka muda ulio wekwa. Hakika muda wa Mwenyezi Mungu utapo fika haucheleweshwi. Laiti mngejua!
قَالَ رَبِّ إِنِّي دَعَوْتُ قَوْمِي لَيْلًا وَنَهَارًا
( 5 ) ![Swahili - Nooh - Aya 5 Nooh - Aya 5](style/islamic/icons/mp3.png)
Akasema: Ee Mola wangu Mlezi! Hakika mimi nimewaita watu wangu usiku na mchana,
فَلَمْ يَزِدْهُمْ دُعَائِي إِلَّا فِرَارًا
( 6 ) ![Swahili - Nooh - Aya 6 Nooh - Aya 6](style/islamic/icons/mp3.png)
Lakini wito wangu haukuwazidisha ila kukimbia.
وَإِنِّي كُلَّمَا دَعَوْتُهُمْ لِتَغْفِرَ لَهُمْ جَعَلُوا أَصَابِعَهُمْ فِي آذَانِهِمْ وَاسْتَغْشَوْا ثِيَابَهُمْ وَأَصَرُّوا وَاسْتَكْبَرُوا اسْتِكْبَارًا
( 7 ) ![Swahili - Nooh - Aya 7 Nooh - Aya 7](style/islamic/icons/mp3.png)
Na hakika mimi kila nilipo waita ili upate kuwaghufiria, walijiziba masikio yao kwa vidole vyao, na wakajigubika nguo zao, na wakakamia, na wakatakabari vikubwa mno!
ثُمَّ إِنِّي دَعَوْتُهُمْ جِهَارًا
( 8 ) ![Swahili - Nooh - Aya 8 Nooh - Aya 8](style/islamic/icons/mp3.png)
Tena niliwaita kwa uwazi,
ثُمَّ إِنِّي أَعْلَنتُ لَهُمْ وَأَسْرَرْتُ لَهُمْ إِسْرَارًا
( 9 ) ![Swahili - Nooh - Aya 9 Nooh - Aya 9](style/islamic/icons/mp3.png)
Kisha nikawatangazia kwa kelele, tena nikasema nao kwa siri.
فَقُلْتُ اسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ إِنَّهُ كَانَ غَفَّارًا
( 10 ) ![Swahili - Nooh - Aya 10 Nooh - Aya 10](style/islamic/icons/mp3.png)
Nikasema: Ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi; hakika Yeye ni Mwingi wa kusamehe.
يُرْسِلِ السَّمَاءَ عَلَيْكُم مِّدْرَارًا
( 11 ) ![Swahili - Nooh - Aya 11 Nooh - Aya 11](style/islamic/icons/mp3.png)
Atakuleteeni mvua inyeshe mfululizo.
وَيُمْدِدْكُم بِأَمْوَالٍ وَبَنِينَ وَيَجْعَل لَّكُمْ جَنَّاتٍ وَيَجْعَل لَّكُمْ أَنْهَارًا
( 12 ) ![Swahili - Nooh - Aya 12 Nooh - Aya 12](style/islamic/icons/mp3.png)
Na atakupeni mali na wana, na atakupeni mabustani na atakufanyieni mito.
مَّا لَكُمْ لَا تَرْجُونَ لِلَّهِ وَقَارًا
( 13 ) ![Swahili - Nooh - Aya 13 Nooh - Aya 13](style/islamic/icons/mp3.png)
Mna nini hamweki heshima ya Mwenyezi Mungu?
وَقَدْ خَلَقَكُمْ أَطْوَارًا
( 14 ) ![Swahili - Nooh - Aya 14 Nooh - Aya 14](style/islamic/icons/mp3.png)
Na hali Yeye kakuumbeni daraja baada ya daraja?
أَلَمْ تَرَوْا كَيْفَ خَلَقَ اللَّهُ سَبْعَ سَمَاوَاتٍ طِبَاقًا
( 15 ) ![Swahili - Nooh - Aya 15 Nooh - Aya 15](style/islamic/icons/mp3.png)
Kwani hamwoni jinsi Mwenyezi Mungu alivyo ziumba mbingu saba kwa matabaka?
وَجَعَلَ الْقَمَرَ فِيهِنَّ نُورًا وَجَعَلَ الشَّمْسَ سِرَاجًا
( 16 ) ![Swahili - Nooh - Aya 16 Nooh - Aya 16](style/islamic/icons/mp3.png)
Na akaufanya mwezi ndani yake uwe nuru, na akalifanya jua kuwa taa?
وَاللَّهُ أَنبَتَكُم مِّنَ الْأَرْضِ نَبَاتًا
( 17 ) ![Swahili - Nooh - Aya 17 Nooh - Aya 17](style/islamic/icons/mp3.png)
Na Mwenyezi Mungu amekuotesheni katika ardhi kama mimea.
ثُمَّ يُعِيدُكُمْ فِيهَا وَيُخْرِجُكُمْ إِخْرَاجًا
( 18 ) ![Swahili - Nooh - Aya 18 Nooh - Aya 18](style/islamic/icons/mp3.png)
Kisha atakurudsheni humo na atakutoeni tena.
وَاللَّهُ جَعَلَ لَكُمُ الْأَرْضَ بِسَاطًا
( 19 ) ![Swahili - Nooh - Aya 19 Nooh - Aya 19](style/islamic/icons/mp3.png)
Na Mwenyezi Mungu amekukunjulieni ardhi kama busati.
لِّتَسْلُكُوا مِنْهَا سُبُلًا فِجَاجًا
( 20 ) ![Swahili - Nooh - Aya 20 Nooh - Aya 20](style/islamic/icons/mp3.png)
Ili mtembee humo katika njia zilizo pana.
قَالَ نُوحٌ رَّبِّ إِنَّهُمْ عَصَوْنِي وَاتَّبَعُوا مَن لَّمْ يَزِدْهُ مَالُهُ وَوَلَدُهُ إِلَّا خَسَارًا
( 21 ) ![Swahili - Nooh - Aya 21 Nooh - Aya 21](style/islamic/icons/mp3.png)
Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika hao wameniasi, na wamemfuata yule ambaye mali yake na wanawe hawakumzidishia ila khasara.
وَمَكَرُوا مَكْرًا كُبَّارًا
( 22 ) ![Swahili - Nooh - Aya 22 Nooh - Aya 22](style/islamic/icons/mp3.png)
Na wakapanga vitimbi vikubwa.
وَقَالُوا لَا تَذَرُنَّ آلِهَتَكُمْ وَلَا تَذَرُنَّ وَدًّا وَلَا سُوَاعًا وَلَا يَغُوثَ وَيَعُوقَ وَنَسْرًا
( 23 ) ![Swahili - Nooh - Aya 23 Nooh - Aya 23](style/islamic/icons/mp3.png)
Na wakasema: Msiwaache miungu yenu, wala msimwache Wadda wala Suwaa' wala Yaghutha, wala Yau'qa, wala Nasra.
وَقَدْ أَضَلُّوا كَثِيرًا ۖ وَلَا تَزِدِ الظَّالِمِينَ إِلَّا ضَلَالًا
( 24 ) ![Swahili - Nooh - Aya 24 Nooh - Aya 24](style/islamic/icons/mp3.png)
Na hao walikwisha wapoteza wengi, wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.
مِّمَّا خَطِيئَاتِهِمْ أُغْرِقُوا فَأُدْخِلُوا نَارًا فَلَمْ يَجِدُوا لَهُم مِّن دُونِ اللَّهِ أَنصَارًا
( 25 ) ![Swahili - Nooh - Aya 25 Nooh - Aya 25](style/islamic/icons/mp3.png)
Basi kwa ajili ya makosa yao waligharikishwa wakaingizwa Motoni, wala hawakuwapata wa kuwanusuru badala ya Mwenyezi Mungu.
وَقَالَ نُوحٌ رَّبِّ لَا تَذَرْ عَلَى الْأَرْضِ مِنَ الْكَافِرِينَ دَيَّارًا
( 26 ) ![Swahili - Nooh - Aya 26 Nooh - Aya 26](style/islamic/icons/mp3.png)
Na Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Usimwache juu ya ardhi mkaazi wake yeyote katika makafiri!
إِنَّكَ إِن تَذَرْهُمْ يُضِلُّوا عِبَادَكَ وَلَا يَلِدُوا إِلَّا فَاجِرًا كَفَّارًا
( 27 ) ![Swahili - Nooh - Aya 27 Nooh - Aya 27](style/islamic/icons/mp3.png)
Hakika ukiwaacha watawapoteza waja wako, wala wao hawatazaa ila waovu makafiri.
رَّبِّ اغْفِرْ لِي وَلِوَالِدَيَّ وَلِمَن دَخَلَ بَيْتِيَ مُؤْمِنًا وَلِلْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَلَا تَزِدِ الظَّالِمِينَ إِلَّا تَبَارًا
( 28 ) ![Swahili - Nooh - Aya 28 Nooh - Aya 28](style/islamic/icons/mp3.png)
Mola wangu Mlezi! Nighufirie mimi na wazazi wangu, na kila aliye ingia nyumbani mwangu kuwa ni mwenye kuamini, na Waumini wote wanaume, na Waumini wanawake. Na wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.